عَنْ عِمْرَانَ بْنِ حُصَيْنٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، قَالَ: دَخَلْتُ عَلَى النَّبِيِّ ﷺ، وَعَقَلْتُ نَاقَتِي بِالْبَابِ، فَأَتَاهُ نَاسٌ مِنْ بَنِي تَمِيمٍ فَقَالَ: «اقْبَلُوا البُشْرَى يَا بَنِي تَمِيمٍ»، قَالُوا: قَدْ بَشَّرْتَنَا فَأَعْطِنَا، مَرَّتَيْنِ، ثُمَّ دَخَلَ عَلَيْهِ نَاسٌ مِنْ أَهْلِ اليَمَنِ، فَقَالَ: «اقْبَلُوا البُشْرَى يَا أَهْلَ اليَمَنِ، إِذْ لَمْ يَقْبَلْهَا بَنُو تَمِيمٍ»، قَالُوا: قَدْ قَبِلْنَا يَا رَسُولَ اللَّهِ، قَالُوا: جِئْنَاكَ نَسْأَلُكَ عَنْ هَذَا الأَمْرِ. قَالَ: «كَانَ اللَّهُ وَلَمْ يَكُنْ شَيْءٌ غَيْرُهُ، وَكَانَ عَرْشُهُ عَلَى المَاءِ، وَكَتَبَ فِي الذِّكْرِ كُلَّ شَيْءٍ، وَخَلَقَ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضَ» فَنَادَى مُنَادٍ: ذَهَبَتْ نَاقَتُكَ يَا بْنَ الحُصَيْنِ، فَانْطَلَقْتُ، فَإِذَا هِيَ يَقْطَعُ دُونَهَا السَّرَابُ، فَوَاللَّهِ لَوَدِدْتُ أَنِّي كُنْتُ تَرَكْتُهَا.

Kutoka kwa Imran bin Huswein, Mwenyezi Mungu awe radhi nao, amesema

Niliingia kwa Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) nikamuacha ngamia wangu mlangoni.Wakamjia Mtume baadhi ya watu katika familia ya Tamim, akawaambia: “pokeeni bishara enyi familia ya Tamim.”Wakasema familia ya Tamim: Umetubashiria, basi tupe mara mbili.Kisha wakaingia baadhi ya watu wa Yemen, Mtume akasema: pokeeni Bishara enyi watu wa Yemen, kwani familia ya Tamim hawakuikubali”.Wakasema watu wa Yemen: Tumeikubali, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu.Wakasema watu wa Yemen: Tumekuja kukuuliza kuhusu hili jambo (la Uislamu).Akasema Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake): “Mwenyezi Mungu alikuwepo, wakati hakuna chochote kilicho kuwepo ispokuwa yeye.Na Kiti chake cha enzi kilikuwa juu ya maji.Na akaandika katika kitabu kila kitu.Na akaumba mbingu na ardhi”.Akaita Muitaji akasema: Ngamia wako ametoweka, ewe Ibn al-Huswein, basi nikaondoka mbio nikimtafuta, Ghafla nikamuona akitokomea kwa umbali.Wallahi, nikatamani laiti ningemuacha”

Muhtasari wa Maana

Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) anaeleza kuhusu baadhi ya mambo ya siri yanayobainisha sifa na matendo ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na ameeleza kuwa Mwenyezi Mungu alikuwa wa milele kabla ya kila kitu, na arshi yake ilikuwa juu ya maji kabla ya kuumba mbingu na ardhi. Kisha akasema kuwa Mwenyezi Mungu aliandika katika Kitabu kilichohifadhiwa, makadirio ya waja na matukio yote, baada ya hapo akaumba Mbingu na Ardhi.

Miradi ya Hadithi