عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه، عَنِ النَّبِيِّ ﷺ، قَالَ: «اجْتَنِبُوا السَّبْعَ المُوبِقَاتِ» قَالُوا: يَا رَسُولَ اللَّهِ، وَمَا هُنَّ؟ قَالَ: وَالسِّحْرُ، وَقَتْلُ النَّفْسِ الَّتِي حَرَّمَ اللَّهُ إِلَّا بِالحَقِّ، وَأَكْلُ الرِّبَا، وَأَكْلُ مَالِ اليَتِيمِ، وَالتَّوَلِّي يَوْمَ الزَّحْفِ، وَقَذْفُ المُحْصَنَاتِ المُؤْمِنَاتِ الغَافِلاَتِ». 

00:00
00:00
تحميل الملف الصوتي

Kutoka kwa Abu Huraira, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kutoka kwa Mtume, swallallahu alayhi wa sallam, ambaye amesema: 1- “Jiepusheni na madhambi saba yenye kuangamiza.” Wakasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, na ni yapi? Akasema Mtume: 2- “Kumshirikisha Mwenyezi Mungu, 3- Na uchawi, 4- Kuiua nafsi aliyoiharamisha Mwenyezi Mungu, isipokuwa kwa uadilifu. 5- Kula riba 6- Kula pesa za yatima 7- Kuikimbia vita 8- Na kuwatuhumu na machafu wanawake walio safi, Waumini walioghafilika”

Muhtasari wa Maana

Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam anatahadharisha juu ya madhambi makubwa hatari kwa waja, ambayo ni: Shirki, uchawi, kuua pasina haki, riba, pesa ya mayatima, kukimbia vita, na kuwatukana wanawake walio safi

Miradi ya Hadithi