عَنْ أَبِي مُوسَى الْأَشْعَرِيّ رضى الله عنه، قَالَ: قَامَ فِينَا رَسُولُ اللهِ بِخَمْسِ كَلِمَاتٍ، فَقَالَ: «إِنَّ اللهَ - عزَّ وجلَّ - لَا يَنَامُ،  « وَلَا يَنْبَغِي لَهُ أَنْ يَنَامَ، يَخْفِضُ الْقِسْطَ وَيَرْفَعُهُ، يُرْفَعُ إِلَيْهِ عَمَلُ اللَّيْلِ قَبْلَ عَمَلِ النَّهَارِ، وَعَمَلُ النَّهَارِ قَبْلَ عَمَلِ اللَّيْلِ، حِجَابُهُ النُّورُ - وَفِي رِوَايَةٍ: النَّارُ - لَوْ كَشَفَهُ لَأَحْرَقَتْ سُبُحَاتُ وَجْهِهِ مَا انْتَهَى إِلَيْهِ بَصَرُهُ مِنْ خَلْقِهِ».

Kutoka kwa Abu Musa al-Ash’ariy, (Radhi Za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema: siku moja Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na Amani ziwe juu yake) alisimama na kutueleza mambo matano, akasema:“Hakika Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu na Mtukufu, halali usingizi.Wala hahitajii kulala,Anashusha mizani na kuinyanya.Matendo yote yanayo tendeka usiku hupelekwa kwake kabla ya Matendo ya mchana, na Matendo yote yanayo tendeka mchana hupelekwa kwake kabla ya Matendo ya usiku.Kizuizi (kati yake na viumbe wake) ni Nuru - na katika riwaya: Moto.Akiondoa kizuizi hicho, Utukufu wa uso wake utachoma kila kiumbe ataefikiwa na macho yake katika viumbe wake”

Related by Muslim, 179.

Miradi ya Hadithi