2 - KUSHUHUDIA KUWA HAPANA MOLA APASAE KUABUDIWA KWA HAKI ISPOKUWA ALLAH:

عَن مُعاذِ بنِ جبلٍ ‏‏رضى الله عنه قال:كنتُ رَدِيفَ النبيِّ ﷺ على حمارٍ، فقال: «يا معاذُ!، أتدري ما حقُّ اللهِ على العبادِ؟ وما حقُّ العبادِ على اللهِ؟» قلتُ: اللهُ ورسولُه أعلمُ. قال: «فإنَّ حقَّ الله على العبادِ أن يعبدوه ولا يُشركوا به شيئًا.وحقَّ العباد على الله أن لا يُعذِّب مَن لا يُشرك به شيئًا».قلتُ: يا رسول الله، أفلا أُبشِّر الناس؟ قال: «لا تُبَشِّرْهم فيتَّكلوا» متفق عليه.

Kutoka kwa Mua’dh ibn Jabal (r.a) amesema:

1. Nilikuwa nimepanda nyuma ya Mtume (s.a.w) katika mnyama. 

2. Akasema Mtume (s.a.w): “ewe Mua’dh! Je, wajuwa ni ipi haki ya Mwenyezi Mungu kwa waja wake? na ni ipi haki ya waja kwa Mwenyezi Mungu”?  3.Nikasema: Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndio wajuzi zaidi juu ya hilo. 4.Akasema Mtume (s.a.w): “hakika haki ya Mwenyezi Mungu juu ya waja wake ni kumuabudu yeye peke yake wala wasimshirikishe na chochote 5. Na haki ya waja juu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kutomuadhibu yeyote asiemshirikisha na chochote” 

6.Nikasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, je nisiwabashirie watu? Akasema Mtume rehma na amani ziwe juu yake: “Hapana usiwape bishara hii, kwani watakuwa wavivu”

Miradi ya Hadithi