عن أبي هُرَيرة رضى الله عنه قال: قال رسول الله«أنا أَوْلى الناس بعِيسى بنِ مَريمَ في الدنيا والآخرةِ، والأنبياءُ إِخْوَةٌ لِعَلَّاتٍ؛ أمهاتُهم شتَّى، ودِينُهم واحدٌ»، وفي رواية: «ليس بَيْني وبينَه نَبِيٌّ».

Kutoka kwa Abu Musa al-Ash’ariy, (Radhi Za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema: siku moja Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na Amani ziwe juu yake) alisimama na kutueleze mambo matano, akasema:

  • “Hakika Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu na Mtukufu, halali usingizi. Wala hahitajii kulala, Anashusha mizani na kuinyanya.
  • Matendo yote yanayo tendeka usiku hupelekwa kwake kabla ya Matendo ya mchana, na Matendo yote yanayo tendeka mchana hupelekwa kwake kabla ya Matendo ya usiku. Kizuizi (kati yake na viumbe wake) ni Nuru - na katika riwaya: Moto. Akiondoa kizuizi hicho, Utukufu wa uso wake utachoma kila kiumbe ataefikiwa na macho yake katika viumbe wake” ( Muslim (179).

Muhtasari wa Maana

Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) aliwaeleza maswahaba zake baadhi ya sifa za Mwenyezi Mungu Mtukufu, miongoni mwa sifa hizo ni kutolala usingizi, na kwamba usingizi ni jambo lisilofaa kwa Mola Mtukufu, kwa sababu usingizi ni sifa ya upungufu, na Mwenyezi Mungu ametakasika na sifa yoyote ya upungufu. Anayakubali matendo mema na kuyanyanyua kwake na kuyakataa maovu na kuwarejeshea, na Malaika hupandisha kwake matendo ya usiku kabla ya kuanza kuandika matendo ya mchana, na hupandisha kwake matendo ya mchana kabla ya kuanza kuandika matendo ya usiku. Na kwamba pazia lake limetokana na Nuru - au Moto - ikiwa pazia hilo lingeondolewa, basi nuru hiyo tukufu itachoma viumbe vyote.

Miradi ya Hadithi